Page Nav

HIDE

Grid

GRID_STYLE

Classic Header

{fbt_classic_header}

Header Ad

//

Breaking News

latest

UFUGAJI WA NGURUWE : MBINU ZA KUFUGA KIBIASHARA

Ufugaji wa Nguruwe  ni kati ya shughuli zinazokua haraka katika Afrika Mashariki na ya Kusini. Ukuaji wa miji na ongezeko la watu kumeendana...

Ufugaji wa Nguruwe ni kati ya shughuli zinazokua haraka katika Afrika Mashariki na ya Kusini. Ukuaji wa miji na ongezeko la watu kumeendana na ongezeko kubwa la mahitaji ya protini ya wanyama. Uwezo wa kukua haraka, ubora wa nyama kiafya na ladha nzuri inatoa nafasi kubwa ya maendeleo ya ufugaji wa nguruwe kama chanzo cha kipato kwa mfugaji. Kijarida hiki kinatoa mwongozo kuhusu mahitaji muhimu ya ufugaji nguruwe, mbinu za kuboresha uzalishaji, kudhibiti magonjwa na pia mwongozo wa kujali haki za nguruwe kama kiumbe hai kinachoweza kusikia maumivu kisipotendewa kinavyostahili. Nguruwe ana gharama ndogo za matunzo, anatoa mafuta, huleta kipato cha pesa, hutoa mbolea ya mimea. Faida ya ufugaji nguruwe hutegemea zaidi ubora wa matunzo. Vile vile kumbuka kutumia vyanzo nafuu vya chakula na kujengea miudombinu. Msomaji anashauriwa kuwaona wataalamu kwa ushauri zaidi na pia kusoma vitabu vya rejea kuhusu ufugaji nguruwe



NGURUWE ni mnyama msafi sana na mwenye akili. Akipewa banda lenye nafasi ya kutosha huweza kuchagua sehemu ya kulala, kujisaidia na akauweka mwili wake katika hali ya usafi sana. U safi wa banda na mazingira utakuhakikishia nguruwe wasafi bila uchafuzi wa mazingira kama tunavyoona kwa wafugaji wengi mijini na vijijini. Tenga mavazi na viatu maalumu kwa ajili ya kazi za nguruwe na oga vizuri baada ya kufanya kazi kwenye mabanda ya nguruwe kwa muda mrefu.

                             Nyumba ya nguruwe

 Kwa ujumla nyumba za aina mbili huhitajika katika ufugaji wa nguruwe 

 1.Nyumba za kukuzia na kunenepesha nguruwe wa kuchinja 

2. Nyumba za nguruwe wazazi

Sifa za msingi za nyumba bora ya nguruwe

Nyumba ijengwe eneo lenye kivuli cha kutosha

• Nyumba iwe na nafasi ya kutosha

• Ijengwe sehemu yen ye mwinuko kiasi ili kuwezesha maji kuondoka kwa urahisi

• Iwe na chombo/kihori cha kuweka chakula na kingine chakuweka maji

• Iwe na sakafu imara iliyotengenezwa kwa saruji, mabanzi, miti na isiwe na unyevu

• Sakafu ya saruji iwe na mteremko (slope) inayoweza kuondoa uchafu kwa urahisi

ndani ya banda.

• Sakafu ya mabanzi, mbao au miti iwe inatoa nafasi ya kuondoa uchafu kama kinyesi

ndani ya banda.

• Iwe na mtaro wa kuondolea maji, mkojo na kinyesi hadi shimo la kutunzia

• Kuta za mabanda ya nguruwe zinatakiwa kuwa imara, ziwe na uwezo wa kuwasitiri

nguruwe wasitoke nje

• Iweze kuingiza hewa ya kutosha ndani ya banda hasa kama ukuta umezibwa (solid walls)





      Upate wapi Nguruwe wa Kufuga

Nunua nguruwe wa kufuga kutoka kwenye mashamba au wafugaji wanaoaminika ukizingatia

yafuatayo.

• Usizalishe nguruwe wanaotokana na ukoo mmoja yaani ndugu kama kaka ria dada.

Nunua dume na jike toka mahali tofauti.

• Tumia ushauri wa wataalamu kuchagua nguruwe bora

Sifa za kuangalia kwa nguruwe bora wa mbegu

• Nguruwe wa mbegu awe na sifa ya kukua haraka na asiwe na ulemavu wa aina yeyote, na

hasa wa miguu kwa dume.

Mama mzazi wa nguruwe awe na historia ya kuzaa watoto 10 hadi 12 kwa mzao mmoja

• Jike awe na chuchu zaidi ya 12.

• Dume awe na sehemu za kiume yaani korodani na uume unaoonekana sawa sawa. Pia awe

na hamu ya kupanda majike.

            Mbinu za uzalishaji

Matunzo ya dume la uzalishaji 

Chagua dume la mbegu bora, lisilokuwa na kilema au ugonjwa wowote.Tenganisha dume na majike ili kuepusha kupandwa kusiko  na kumbukumbu. Dume la nguruwe halipaswi kunenepa, kwa hiyo usimlishe chakula kingi na mpatie mazoezi ya kutosha asije akawa mvivu

 • Nguruwe dume anaanza kupanda majike akiwa na umri wa miezi 4 hadi miezi 9. Dume liruhusiwe kupanda mara moja tu kwa kila juma. Anapofika miezi 10 anaweza kupanda mara mbili hadi mara tatu kwa wiki. Akiwa na mwaka mmoja na zaidi anaweza kupanda kila siku kwa majuma mawili hadi matatu, kisha apumzike kwa majuma mawili. Ni vizuri nguruwe dume mmoja apande majike 15 hadi 20 kwa mwaka. 

• Madume madogo yapande majike madogo, dume kubwa likimpanda jike dogo anaweza akamletea maradhi ya mgongo. Ni muhimu kupandisha dume kabla hajala chakula, na asitumiwe mara tu baada ya chakula iii asiwe mvivu


  Utunzaji nguruwe mwenye mimba

Mimba ya nguruwe huchukuwa miezi mitatu (3) wiki tatu(3) na siku tatu(3) yaani siku 114

• Nguruwe mwenye mimba apewe chakula cha kutosha kiongezwe polepole tokea posho ya kawaida hadi kilo 3 - 3. 5 kwa siku

Matayarisho ya nyumba kabla ya kuzaa

Osha banda la kuzalia kwa maji na kuliacha likauke

• Tandika nyasi kavu mara baada ya nyumba kukauka

• Ongeza taa ya chemli au umeme kama uko mikoa yenye baridi kwenye sehemu ya vitoto.

• Tengeneza sehemu ya kuzalia kwa mbao au mabomba

Kumuandaa nguruwe mama kabla ya kuzaa

Mpe dawa ya rninyoo siku 10 kabla ya kuzaa

• Mogeshe mama nguruwe kwa sabuni ya mkono na brashi

• Muhamishie katika chumba cha kuzalia siku 7 kabla hajazaa

• Mpunguzie lishe siku 2 kabla ya kuzaa

• Siku ya kuzaa mpe nguruwe maji ya kunywa tu

               Upandishaji jike

Kati ya siku nne hadi saba baada ya kuachishwa watoto, nguruwe mama hupata joto.

Nguruwe jike alie kwenye joto apelekwe kwenye banda la dume na sio kinyume chake. Rudia

kumpandishajike alie kwenye joto masaa 12 baada ya mpando wa kwanza; rudia

kumpandisha mara 2 hadi 4. Kamajike hatarudia kwenye joto baada ya wiki 3 atakuwa

ameshika mimba

 

Dalili za joto

• Sehemu ya uzazi kubadilika na kuwa nyekundu

• Nguruwe hatulii na hukojoa mara kwa mara

• Ute kama makamasi hutoka sehemu za siri

• Nguruwe mwenye joto hujaribu kuwapanda wenzake na yeye akipandwa hutulia

 

UTUNZAJI WA VITOTO VYA NGURUWE

Ulishaji wa maziwa ya kwanza

Baada ya kuzaliwa na kusafishwa, hakikisha vitoto vinanyonyeshwa. Vitovu viwekewe dawa (Iodine

5%) iii kuzuia magonjwa. Kama mama amefariki mara tu baada ya kuzaa na hakuna nguruwe

mwingine anayeweza kunyonyesha; tumia maziwa ya ng'ombe. ongeza sukari na yai bichi koroga na

uwanyonyeshe kwa kutumia chupa ya maziwa ya mtoto.

Joto

Vitoto vya nguruwe havizaliwi na manyoya na hawana mafuta mengi ya kutosha kuwaletea joto

mwilini; hivyo ni rahisi kufa kwa baridi. Tumia taa ya stimu au chemli kuongeza joto.

Kuzuia upungufu wa damu

Maziwa ya nguruwe yana upungufu wa madini ya chuma yaongezayo damu. Hivyo baada ya

majuma mawili au matatu watoto huanza kudhoofu kwa kukosa madini hayo mwilini. Kuondoa

tatizo hili inabidi vitoto vidungwe sindano ya madini kwenye misuli siku mbili au tatu tangu

kuzaliwa. Kama sindano haipatikani njia nyingine za kuwapatia watoto madini hayo ni kwa kuwapa

vidonge vya madini chuma, au kuwapa madini hayo kwen_ e ndimi zao au chuchu za mama yao siku

mbila hadi tatu baada ya kuzaliwa

Ukataji meno

Siku chache kabla ya kuzaliwa,meno yaliochongoka kama sindano huchomoza katika taya mbili.Meno hayo humuumiza mama wakati watoto wanaponyonya,matokeo yake mama hupiga watoto mateke.Hii husababisha vifo vya watoto kutokana na kupigwa na kukosa maziwa ya mwanzi hivyo inabidi kupunguza madhara hayo

 

Chakula bora kwa nguruwe ni moja ya mahitaji muhimu sana kwenye dhana nzima ya ufugaji wa

nguruwe wenye tija na faida kwa mfugaji. Chakula cha nguruwe kinagharimu yapata asilimia hamsini

sabini ya gharama zote za ufugaji wa nguruwe. Kati ya matatizo mengi yanayosababisha tija na

ufanisi duni wa uzalishaji wa nguruwe yanatokana na lishe duni. Nguruwe wakipatiwa lishe bora, tija

na ufanisi wa uzalishaji utakuwa mkubwa hivyo kuongeza faida kwa mfugaji.

Kuachisha kunyonyesha

• Viachishe vitoto kunyonya wakifikia umri wa miezi miwili wanapokuwa na uzito wa kilo 10.

Siku ya kuachisha kunyoyesha muondoe mama nguruwe kwa watoto wake na kumuweka

chumba kingine

• Mpe mama chakula cha kutosha

Kuhasi

Vitoto ambavyo havihitajiki kwa ajili ya kizazi bora katika mfugo, vihasiwe vikiwa katika juma la

tatu hadi la nne. Nguruwe walio hasiwa huwa wapole, wenye nguvu, wazito na nyama yao haina

harufu ya dume. Bwana mifugo atakupa maelezo zaidi kuhusujinsi ya kufanya.

 

Baadhi ya faida za lishe bora kwa nguruwe ni:

1. Lishe bora huharakisha ukuaji wa haraka wa nguruwe na hivyo kupata uzito unaohitajika kwa

kipindi kifupi.

2. Lishe bora hupunguza gharama za ufugaji na hivyo kuongeza faida kwa mfugaji kwa sababu

nguruwe atahitaji kiasi kidogo tu cha chakula na atachukua muda mfupi kupata uzito mkubwa

3. Lishe bora itapunguza maambukizi ya magonjwa.

4. Lishe bora huongeza kiasi cha mayai yatakayoivishwa na mama nguruwe na hivyo kuongeza idadi

ya watoto watakaozaliwa

5. Lishe bora huongeza kiasi cha maziwa yatakayotengenezwa na mama nguruwe kwa ajili ya

watoto hivyo kuwafanya wawe na afya bora itakayo wawezesha wakue haraka na kupunguza

idadi ya vifo kwa watoto.

6. Lishe bora inaongeza ufanisi wa madume ya nguruwe na hivyo kuongeza uwezo wa kupanda

. Viini lishe muhimu kwenye lishe ya nguruwe

Nguruwe wana uwezo wa kula aina nyingi za vyak:ula lakini vyenye uwezo wa kumeng'enywa kwa

urahisi. Chakula cha nguruwe kilichokamilika kinahitaji kuwa na mchanganyiko wa viini lishe vitano,

navyo ni

1. Vyakula vyenye kutia nguvu mwilini (kama pumba za mahindi, ngano, mchele)

2. Vyakula vya kujenga mwili (kama mashudu ya alizeti, pamba, unga wa dagaa)

3. Vyakula vya asili ya madini (kama chumvi, chokaa, mifupa iliosagwa)

4. Vyak:ula vya asili ya vitamini (kama majani mabichi, mbogamboga na matunda)

5. Maji

Baadhi ya faida za lishe bora kwa nguruwe ni:

1. Lishe bora huharakisha ukuaji wa haraka wa nguruwe na hivyo kupata uzito unaohitajika kwa

kipindi kifupi.

2. Lishe bora hupunguza gharama za ufugaji na hivyo kuongeza faida kwa mfugaji kwa sababu

nguruwe atahitaji kiasi kidogo tu cha chakula na atachukua muda mfupi kupata uzito mkubwa

3. Lishe bora itapunguza maambukizi ya magonjwa.

4. Lishe bora huongeza kiasi cha mayai yatakayoivishwa na mama nguruwe na hivyo kuongeza idadi

ya watoto watakaozaliwa

5. Lishe bora huongeza kiasi cha maziwa yatakayotengenezwa na mama nguruwe kwa ajili ya

watoto hivyo kuwafanya wawe na afya bora itakayo wawezesha wakue haraka na kupunguza

idadi ya vifo kwa watoto.

6. Lishe bora inaongeza ufanisi wa madume ya nguruwe na hivyo kuongeza uwezo wa kupanda

7. Vyakula na ulishaji

Chakula bora kwa nguruwe ni moja ya mahitaji muhimu sana kwenye dhana nzima ya ufugaji wa

nguruwe wenye tija na faida kwa mfugaji. Chakula cha nguruwe kinagharimu yapata asilimia hamsini

sabini ya gharama zote za ufugaji wa nguruwe. Kati ya matatizo mengi yanayosababisha tija na

ufanisi duni wa uzalishaji wa nguruwe yanatokana na lishe duni. Nguruwe wakipatiwa lishe bora, tija

na ufanisi wa uzalishaji utakuwa mkubwa hivyo kuongeza faida kwa mfugaji.


 Jinsi ya kutengeneza chakula cha nguruwe

Wakati wa kutengeneza chakula cha nguruwe inabidi kuzingatia yafuatayo:

• Mchanganyiko wake uwe na viinilishe vinne vilivyotajwa hapo juu

• Chagua aina ya viinilishe vinavyoweza kupatikana kwa urahisi na bei nafuu kwenye mazingira

yako

• Aina ya mchanganyiko wa chakula ni muhimu uzingatie mahitaji ya nguruwe kama umri (mfano:

nguruwe wanaonyonya, waliochishwa kunyonya, wanaokua, na wanaonyonyesha)

Kiasi na namna ya kulisha

Nguruwe wanahitajika kulishwa aina hii ya chakula mara mbili (asubuhi na mchana) au zaidi kwa

siku

• Kiwango/kiasi cha kulisha kwa nguruwe wa aina na rika tofauti kimeonyeshwa kwenye jedwali

Namba3

• Pamoja na vyakula vilivyotajwa, wafugaji wanashauriwa kuwapatia nguruwe vyakula vyao vya

kijadi kama vyakula vya ziada mfano, majani mabichi laini, majani ya maboga, mbogamboga,

matunda kama maparachichi, majani ya viazi n.k

BILA SHAKA UMEPATA KITU

Acha maoni yako hapo chini,AHSANTE

No comments