SOKA : WAFAHAMU WACHEZAJI 5 WENYE MAJINA MAREFU SANA Imekuwa ni kawaida kusikia majina ya wachezaji pindi wanapotangazwa...
Imekuwa ni kawaida
kusikia majina ya wachezaji pindi wanapotangazwa kupitia Television au Radio
wakati mpira ukichezwa, wengi huwa tunatambua majina ya kawaida na mafupi
kutokana na namna ya matamshi ambayo mtangazaji hutamka. Stori kutoka onebiselumedia hii ndio Top 5 ya majina marefu zaidi kwa wachezaji soka,
huenda wakawepo wengine ila imenifikia list hii.
ni staa
aliyezaliwa Saint Max Ufaransa ambaye jina lake lina jumla ya herufi 36. Kwa
sasa anaitumikia klabu ya Olympiacosinayoshiriki Super League ya Ugiriki,
amewahi pia kuichezea West Ham Unitedya Uingereza, staa huyu huwa anacheza kama
beki wa kati.
Henrique Hilário Meireles Alves Sampaio:
ni mzaliwa
kutoka Ureno ambaye amestaafu kucheza soka, alicheza katika nafasi ya Golikipa,
amebahatika kucheza kwenye timu yake ya taifa na klabu tofauti ikiwemo Chelsea
ya Uingereza. Jina lake lina jumla ya herufi 35.
Fredrik Olof Esaias Stoor Siekkinen:
Fredrik Olof Esaias Stoor Siekkinen:
Anajulikana zaidi
kama Fredrick Stoor ambaye amezaliwa Sweden, kwa sasa anaichezea timu ya Viborg
FF inayoshiriki Danish Superliga ya Denmark. Stoor anacheza kama beki wa kulia.
Ameshawahi kuitumikia klabu ya Fulham ya Uingereza pamoja Derby Country na timu
ya taifa ya Sweden. Jina lake lina herufi 31.
Geovanni Deiberson Maurício Gómez:
Geovanni Deiberson Maurício Gómez:
ni Mbrazil ambaye tayari amestaafu kucheza
soka, anatambulika zaidi kwa jina la Geovanni, alikuwa akicheza kama kiungo
mshambuliaji akiwa na uwezo wa kucheza pia nafasi ya winga. Geovanni amewahi
kuzichezea FC Barcelona, Manchester City, Hull City, Benfica na timu ya taifa
yaBrazil. Jina lake lina jumla ya herufi 30.
Diniyar Rinatovich Bilyaletdinov
Diniyar Rinatovich Bilyaletdinov
jina ambalo
limekuwa likitumika na wengi kumuita, ni mzaliwa kutoka Moscow, Urusi ambaye
hivi sasa anaitumikia timu ya Rubin Kazaninayoshiriki Ligi Kuu Urusi.
Bilyaletdinov amewahi kucheza katika nafasi ya kiungo akiwa na vilabu vya
Locomotive Moscow, Everton na amecheza timu ya taifa ya Urusi. Jina lake lina
herufi 30.
Kaka hayo majina hayawez kuwa dawa ya corona kwelii!! 😂😂😂
ReplyDeleteHahahahah majina marefu kinyama 😝😝😝 ndani yake kuna udawa hahahahah
DeleteHayo majina duh
ReplyDelete