Page Nav

HIDE

Grid

GRID_STYLE

Classic Header

{fbt_classic_header}

Header Ad

//

Breaking News

latest

CORONA VIRUS (COVID-19): WHO - VIFAA VYA KUPIMA CORONA TANZANIA HAVINA SHIDA

Shirika la Afa Duniani  ( WHO)  limeyakataa madai ya rais wa  Tanzania John Magufuli  kwamba kumekuwa na kasoro katika vifaa vya kupimia vir...




Shirika la Afa Duniani ( WHO) limeyakataa madai ya rais wa Tanzania John Magufuli kwamba kumekuwa na kasoro katika vifaa vya kupimia virusi vya corona nchini humo. Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Mkurugenzi wa WHO kwa Afrika Matshidiso Moeti amesema hawakubaliani na kile alichokisema rais Magufuli. Taarifa hiyo inatolewa baada ya Jumapili iliyopita rais huyo wa Tanzania kusema vifaa vya kupima vimekuwa na kasoro, na kubaini kupatikana kwa virusi vya corona katika papai na mbuzi 

Pia Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa Afrika (CDC) nacho kimesema kwamba vifaa vinavyotumika kupimia virusi vya corona nchini Tanzania havina shida yoyote. Leo alhamisi, Mkuu wa Afrika CDC Dkt. John Nkengasong amezungumza na waandishi wa habari kupitia mtandao katika ofisi yake na amenukuliwa akisema;

"Vipimo ambavyo Tanzania inatumia tunajua kwamba vinafanyakazi vizuri!"

Kauli hiyo ya Mkuu wa Africa CDC, inapingana na kauli aliyoitoa  rais wa Tanzania ambaye alisema huenda vipimo hivyo vikawa na matatizo.

Kituo hicho cha Africa CDC pamoja na wakfu wa Jack Ma, Shirika la msaada la bilionea wa China, lilisambaza vifaa hivyo, Nkengasong amesema na kuongeza kwamba vilidhinishwa na wanachojua ni kwamba vinafanya vizuri.

Kituo hicho kiko chini ya Umoja wa Afrika kina majukumu ya kuratibu mapambano dhidi ya mlipuko wa mangonjwa barani Afrika.

source:BBCswahili and DW swahili

 

 


No comments